Timu Yetu Tanzania

Zlatan Milisic

Zlatan Milisic

Mratibu Mkazi
Bwana Milišić analeta uzoefu wa miaka 30 katika kazi za kibinadamu na maendeleo, akifanya kazi na Umoja wa Mataifa katika Asia ya Kati, Kaskazini, Magharibi na Afrika Mashariki, Mashariki ya Kati na Ulaya Mashariki. Kabla ya kuchukua nafasi yake ya sasa kama Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, aliwahi kuwa Mwakilishi wa WFP na Mkurugenzi wa Nchi nchini Afghanistan. Kabla ya hapo, alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Programu na Sera ya WFP huko Roma, Italia. Pia ameshikilia nyadhifa za usimamizi na Umoja wa Mataifa nchini Mali, Libya, Misri, Kyrgyzstan, Tajikistan, Lebanon, Somalia, Burundi, Sudan Kusini na Rwanda. Kabla ya kazi yake na Umoja wa Mataifa, alikuwa mwanasheria katika mazoezi ya kibinafsi. Bwana Milišić ana shahada ya kwanza ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Sarajevo na Shahada ya Uzamili ya Sanaa katika Siasa za Kimataifa na Mafunzo ya Usalama kutoka Chuo Kikuu cha Bradford.
Stephen Bainous Kargbo Profile

Tipo Tito Nyabenyi

FAO
Representative
Mr. Kargbo is the UNIDO representative to Tanzania, Mauritius and the Secretariat of the East African Community (EAC). He has national and international work experience of over 30 years in teaching/research, organizational change and development work. He has held various positions in NGOs, academia and the UN system (UNDP and UNIDO). Before his current position, he worked in the UNIDO Regional Office in Ethiopia, overseeing operations in Burundi, Rwanda and Uganda, as well as activities related to the African Union Commission. Mr. Kargbo holds a B.Sc.in Agricultural Education from the University of Sierra Leone, M.Sc.in Rural Development and PhD in Agricultural Economics from the Georg-August University of Goettingen, Germany.
Maurizio Busatti

Maurizio Busatti

IOM
Mkuu wa Misheni
Bwana Busatti ni raia wa Italia na ana uzoefu wa zaidi ya miongo mitatu ya kufanya kazi kwenye masuala ya wakimbizi na uhamiaji wa kimataifa, ndani ya taasisi za kiserikali, sizizo za kiserikali, Umoja wa Mataifa na sekta binafsi. Alijiunga na IOM mwaka 1996 kufanya kazi ya kuvunja jeshi nchini Angola na tangu wakati huo alishikilia nyadhifa kadhaa katika Makao Makuu na katika misheni za IOM. Alikuwa mratibu wa programu ya kikanda huko Nairobi (1997-2000), kisha akahudumu kama COM nchini Albania (2000-2006) na Uturuki (2006 -2010). Aliteuliwa kuwa mkuu wa Ujumbe Maalum wa Uhusiano nchini Ufaransa (2010-2012), kabla ya kuwa COM nchini Nepal (2012 -2016) ambapo, pamoja na mambo mengine, aliongoza majibu ya IOM kwa tetemeko la ardhi la 2015. Kuanzia mwaka 2016, katika Makao Makuu ya IOM jukumu lake kuu limekuwa kusimamia masuala ya sera na utaratibu yanayohusiana na kuingia rasmi kwa IOM katika mfumo wa Umoja wa Mataifa. Katika jukumu hili alisaidia kuongoza ushirikiano wa IOM ndani ya Umoja wa Mataifa na uwiano wake na Ajenda ya 2030. Bw. Busatti ni mtaalamu wa usimamizi na urejeshaji wa maafa, uhamiaji usio wa kawaida, kazi na maendeleo ya binadamu na msaada wa sera ya uhamiaji. Ana MSc. katika Sayansi ya Siasa na Stashahada ya kuhitimu ya mahusiano ya kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Florence (Italia) na Shahada ya Uzamili katika Utawala wa Ulinzi (MDA) kutoka Chuo Kikuu cha Cranfield na Chuo cha Sayansi cha Kijeshi cha Kifalme (Uingereza).
Peter Malika Profile

Peter Malika

UNCDF
Mkuu Nchini
Ana uzoefu mkubwa wa masuala ya uongozi wa zaidi ya miaka 15 katika maendeleo na biashara ya kimataifa, ana uzoefu na usimamizi wa kikandarasi katika mradi wa bahati 500 unaozingatia ushirika (fortune 500) huko Marekani; usimamizi wa uendeshaji biashara ngazi ya dunia na kikanda; ujuzi katika uwekezaji wenye matokeo chanya, utafutaji fedha kwa shughuli za maendeleo na ufumbuzi. Peter amefanya kazi Umoja wa Mataifa katika nyadhifa mbalimbali katika ngazi ya kitaifa, kikanda na duniani na ameongoza miradi mtambuka ya maendeleo na ubunifu katika maendeleo ya kiuchumi ya mahalia, uhimilivu wa tabianchi, nishati jadidifu, usalama wa chakula, uwezeshaji wanawake kiuchumi, sekta binafsi na uanzishwaji wa masoko ya mitaji, usimamizi wa maarifa na kuhamasisha ushirikiano Afrika na Asia.
Mark Bryan Schreiner Photos

Mark Bryan Schreiner

UNFPA
Mwakilishi
Mark alijiunga na familia ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania akitokea Rwanda, ambako alikuwa na wadhifa kama Mwakilishi wa UNFPA kutoka 2017 hadi 2021. Kwa miongo miwili iliyopita, Mark amefanya kazi Umoja wa Mataifa kama kiongozi wa kipekee na mchechemuzi wa afya na maendeleo ya wanawake na vijana. Amefanya majukumu ya UNFPA katika Ofisi ya Kanda Ndogo ya Pasifiki katika Visiwa vya Fiji, Pakistani, Eritrea, Afrika Kusini, Nigeria na Divisheni ya Afrika katika Makao Makuu ya UNFPA huko New York. Mark pia amewahi kufanya kazi na Mpango wa Umoja wa Mataifa - Mazingira - UNEP nchini Kenya na pia katika Tume ya Uchumi na Jamii ya Umoja wa Mataifa huko Asia na Pasifiki nchini Thailand. Mark ameoa na ni raia wa Canada.
Shalini Bahuguna

Shalini Bahuguna

UNICEF
Mwakilishi
Shalini Bahuguna alishika wadhifa huu wa Mwakilishi wa UNICEF katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzisha (kuanzia) Desemba, 2019. Kabla ya kupokea jukumu hili, Bi. Bahuguna alikuwa Naibu Mwakilishi wa UNICEF huko Ethiopia, jukumu alilokuwa nalo tangu Agosti, 2016. Alijiunga na UNICEF kama Mkuu wa Sera ya Jamii huko Nigeria mwaka 2009 na pia alifanya kazi kama Naibu Mwakilishi wa UNICEF huko Myanmar. Bi. Bahuguna ni mtaalamu wa maendeleo mwenye uzoefu huko Asia na Afrika katika muktadha wa nchi mbalimbali. Alianza maisha yake ya kazi na AZISE ya Maji na Usafi wa Mazingira huko India na kisha kufanya kazi katika Serikali ya India—programu ya magezu ya sekta ya maji chini ya Benki ya Dunia. Ana uzoefu mkubwa kama msimamizi wa misaada na mtaalamu wa maendeleo ya jamii alioupata akifanya kazi na Indara ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID) katika nchi za India, China, Indonesia na Afghanistani.
Hodan Addou Profile

Hodan Addou

UN Women
Mwakilishi
Hodan Addou amekuwa Mwakilishi wa UN Women nchini Tanzania tangu Aprili, 2018. Ana uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika kuhamasisha usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake. Kabla ya kuja Tanzaina, alifanya kazi kama Mwakilishi katika nchi za Uganda, Zimbawe na Sudani. Vile vile alishika wadhifa wa mshauri mwandamizi wa sera, mratibu wa nchi na program za kikanda katika nchi za Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika na pia Makao Makuu huko New York.
Sarah Gordon-Gibson

Sarah Gordon-Gibson

WFP
Mwakilishi
Sarah Gordon-Gibson amekuwa akifanya kazi katika Shirika la Mpango wa Chakula Duniani kwa zaidi ya miaka 20. Alichukua majukumu yake kama Mwakilishi nchini Tanzania mnamo Septemba 2020. Pia aliwahi kuwa Mwakilishi nchini Jordan na Lao PDR. Kabla ya kazi hizi, alikuwa Meneja wa Mpango wa Mkoa wa Kukabiliana na Mgogoro wa Syria, akifunika Misri, Iraq, Jordan, Lebanon, Syria na Uturuki. Kabla ya nafasi yake mashariki ya kati, aliwahi kuwa Naibu Mkurugenzi wa Nchi nchini Niger, Myanmar na Tanzania. Nafasi zake za awali zimekuwa katika nchi za Mauritania, Armenia na Morocco. Ana shahada ya uzamili katika sheria kutoka Chuo Kikuu cha London, na Shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu kutoka Chuo Kikuu cha Paris I, Panthéon-Sorbonne.
Mkuu wa Ofisi ya Mratibu Mkazi

Shabnam Mallick

RCO
Mkuu wa Ofisi ya Mratibu Mkazi
Kabla ya kushika wadhifa huo nchini Tanzania, Bi. Mallick alikuwa Meneja wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Huduma za Miradi (UNOPS) huko Gambia. Vile vile alikuwa Mratibu wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa wa Kudhibiti Janga la UVIKO-19 nchini Gambia. Bi. Mallick ana zaidi ya miaka 18 ya uzoefu wa kazi za maendeleo ya kimataifa, ambapo kati ya hiyo, miaka 12 ameitumia katika nchi zenye migogoro/zilizotoka katika migogoro, na kwa kiasi kikubwa ameshika nyadhifa za uongozi na program mbalimbali katika nchi za kipato cha chini na zile za kipato cha kati, madola yanayoendelea ya visiwa vidogo na nchi zilizo katika mpito. Alikuwa Naibu Mwakilishi Mkazi wa Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP)- (Programu na Uendeshaji) huko Guyana, Bhutan na Korea ya Kaskazini/DPRK.

Bi. Mallick amefanya kazi katika nchi (mbalimbali) zikiwemo Afghanistani, Darfur nchini Sudani (ambako alikuwa Kaimu Mkuu wa Ofisi), Visiwa vya Solomon (kama Ofisa Mkuu na Meneja wa Malengo ya Maendeleo Endelevu – MDG!) huko Pasifiki ya Kusini na Sri Lanka. Bi. Mallick pia amefanya kazi Washington DC katika Benki ya Dunia (Idara ya Kilimo na Maendeleo Vijijini), kwa ajili ya Idara ya USAID ya Ukuaji wa Uchumi na Biashara/Ofisi ya Wanawake katika Maendeleo; na Brookings Institution – Idara ya Sera ya Nje.