Taarifa kwa vyombo vya habari

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani

06 Machi 2024

Katika siku ya wanawake duniani, tunasherehekea wanawake na wasichana duniani kote, na tunawapongeza kwa yote waliyofanikiwa katika kupigania usawa. 

 

Katika siku ya wanawake duniani, tunasherehekea wanawake na wasichana duniani kote, na tunawapongeza kwa yote waliyofanikiwa katika kupigania usawa. 

Wanawake na wasichan wamepata mafanikio makunwa – wameondoa vikwazo, wamevunja fikra potofu na kuchochea maendeleo kuelekea dunia yenye haki zaidi na usawa zaidi. 

Lakini bado wanakabiliwa na vikwazo vikubwa. Mabilioni ya wanawake na wasichana wanakabiliwa na kuenguliwa, ukosefu wa haki na ubaguzi, ilhali janga lililojikita la ukatili dhidi ya wanawake lilikimomonyoa ubinamu.

Dunia yetu inaakisi milenia ya uhusiano wa kimamlaka uliotawaliwa na mfumo dume.

Na maendeleo yanashambuliwa, kwa  haki za wanawake kurudishwa nyuma 

Kwa kiwango cha sasa, usawa wa kisheria utapatikana miaka mia tatu ijayo.

Tunapaswa kusonga mbele haraka.

Katika siku ya wanawake duniani, tunashikamana na wanawake na wasichana wanaopigania haki, na kuazimia kuchagiza maendeleo.

Maudhui ya mwaka huu – wekeza kwa wanawake – yanatumbusha kuwa kutokomeza mfumo dume kunahitaji kuweko kwa fedha mezani.

Tunasaidia mashirika ya wanawake  yaliyo mstari wa mbele.

Na tunapaswa kuwekeza kwenye miradi ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na kuchochea ujumuishaji wanawake na uongozi wa wanawake kwenye uchumi, teknolojia za kidijitali, ujenzi wa amani na hatua kwa tabianchi.

Yote hii inategemea kupatikana kwa fedha kwa ajili ya maendeleo endelevu ili nchi ziwe na fedha za kuwekeza kwa wanawake na wasichana.

Tunahitaji pia kuongeza idadi ya wanawake viongozi kwenye sekta ya biashara, Benki Kuu na Wizara za Fedha. Hii inaweza kusaidia kuchochea uwekezaji kwenye sera na miradi inayokidhi mahitaji ya wanawake na wasichana.

Haki za wanawake zimedhihirisha kuwa njia ya haki ya jamii zenye haki, amani na ustawi. Hii ni vema kwetu sote. 

Kwa Pamoja, hebu na tuchukue hatua za haraka kufanya kuwa halisia.

Asante

Didi Nafisa Profile

Didi Nafisa

RCO
Afisa Habari na Mawasiliano wa Kitaifa
Laurean

Laurean Kiiza

UNDGC
Afisa Kikosi Msaidizi

Mashirika ya UN yanayojihusisha katika Huu Mpango kazi

RCO
Ofisi ya Mratibu Mkazi
UN Women
Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Wanawake
UNDP
Shirika la UN la Mipango ya Maendeleo
UNFPA
Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa
UNIC
Kituo Cha Habari cha Umoja wa Mataifa
UNICEF
Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa

Malengo yanayofanyiwa kazi kupitia mpango huu